Karibu Katika Tovuti ya Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi Zanzibar

STAFF MAIL : Login

Awesome Logo

Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini Zanzibar (Zanzibar Fisheries Research and Marine Resource Institute) – ZAFIRI, ni Taasisi mpya iliyoanzishwa tarehe 23 April, 2019 kwa Hati ya Sheria (Legal Notice) Nambari 32, chini ya kifungu 53 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na kifungu 55 cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Act Nam. 2 ya mwaka 2011 kwa madhumuni ya kuendeleza tafiti za Uvuvi na Maliasili za baharini Zanzibar ili kuimarisha sekta ya Uvuvi, ukulima wa mazao ya baharini na uhifadhi wa mazingira ya Bahari nchini.

Mkurugenzi Mkuu
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini atakua ni mtendaji na msimamizi mkuu wa shughuli za kila siku za Taasisi. Mkurugenzi Mkuu anaeteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa mujibu wa kifungu Na. 24 (1) cha Hati ya Sheria nambari 32 ya kuanzishwa kwa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini Zanzibar.

Dira
Kuwa kituo bora cha utafiti wa uvuvi, maliasili za baharini na sayansi za bahari katika eneo la ukanda wa Magharibi wa Bahari ya Hindi.
Dhamira
Kufanya tafiti za kisasa za uvuvi, rasilimali za bahari na sayansi za bahari, pamoja na kuendeleza mbinu na ubunifu bora ili kutoa muongozo wa matumizi endelevu ya rasilimali za bahari, maendeleo ya sekta za uvuvi na ukulima wa mazao ya baharini, na uhifadhi wa mazingira ya bahari.

Maelezo zaidi

Choose Your Color
You can easily change and switch the colors.