Idara hii inahusika na kudhibiti na kuendeleza shughuli za uvuvi endelevu, kilimo cha mwani, na ufugaji wa viumbe maji kama vile Matango Bahari, Kaa Tope, na Samaki. Idara hii inaongozwa na Mkurugenzi ambae ni mteuliwa wa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.
• Kusimamia, kukuza, kuendeleza, kudhibiti na kufuatilia shughuli za uvuvi endelevu, kilimo cha mwani, na ufugaji wa viumbe maji.
• Kusimamia tathmini mabli mbali za maendeleo ya shughuli za uvuvi na mazao ya baharini.
• Kusimamia na kutekeleza mipango ya utekelezaji wa program za uvuvi na mazao ya baharini ikiwemo takwimu, elimu, nyenzo, miundo mbinu, viwanda, mitaji na masoko.
• Kusimamia ukusanyaji wa tozo na takwimu za uvuvi na mazao ya baharini
• Kuinua uelewa wa jamii juu ya umuhimu wa uvuvi endelevu, miundombinu, zana bora, mitaji na masoko.
• Kusimamia utekelezaji wa sheria na kanuni za uvuvi endelevu.