MAFUTA NA GESI ASILIA
Serikali ya Mapinduzi Zanzibar inaendelea na mchakato wa utafiti, utafutaji na uchimbaji wa mauta na gesi hasa katika ameneo ya bahari Zanzibar. Lakini, licha ya kuwepo kwa taasisi maalumu zinazohusika na utafutaji wa mkondo wa juu wa Mafuta na Gesi Asilia bado kuna changamoto mbali mbali katika kuharakisha upatikanaji wa matunda ya Sekta hii. Ndio maana Serikali kupitia Wizara ya Uchumi wa Buluu na Uvuvi itaendelea kuhakikisha uwepo wa usimamizi bora wa shughuli za mafuta na gesi asilia na kuongeza uwezo wa taasisi zilizopo zinazoshughulikia udhibiti na utafutaji wa mafuta na gesi asilia, ikiwa ni pamoja na kuiongezea Kampuni ya Mafuta ya Zanzibar jukumu la kufanya biashara ya mafuta na gesi asilia kwa mkondo wa chini.
Kwa kuliangalia hilo, Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imeweka vipaumbele vifuatayo vya Uchumi wa Buluu katika Sekta hii:



