ZPRA
Mamlaka ya Udhibiti wa Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia (ZPRA) imeanzishwa chini ya kifungu cha 7 cha Sheria ya Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia nambari 6 ya mwaka 2016. Mamlaka hii imeanza kazi rasmi mwezi Machi 2017 kufuatia kuteuliwa kwa Mkurugenzi Mwendeshaji wa Mamlaka. Lengo la kuanzishwa Mamlaka hii ni kukuza, kusimamia na kudhibiti shughuli za Utafutaji, Uendelezaji na Uzalishaji wa rasilimali za Mafuta na Gesi Asilia kwa eneo la Zanzibar kwa kuzingatia Sheria ya Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia nambari 6 ya mwaka 2016.
Nd. Issa Suleiman Ali
Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji na Utumishi
Kuwa mdhibiti bora wa Sekta ya Mafuta na Gesi Asilia inayochangia kukuza uchumi wa Zanzibar.
Kusimamia, kudhibiti na kukuza shughuli za Utafutaji, Uendelezaji na Uzalishaji wa Mafuta na Gesi Asilia kwa njia endelevu kwa madhumuni ya kukuza uchumi wa Zanzibar.
Kwa mujibu wa Kifungu cha 8(2) cha Sheria ya Utafutaji na Uchimbaji wa Mafuta na Gesi Asilia, majukumu ya ZPRA ni kama yafuatayo:
ZPRA imeundwa na Idara 6 ambazo zimegawika katika jumla ya Divisheni 11 kama zinavyoonekana hapo chini:
Divisheni ya Utafutaji, Uchambuzi wa Masuala ya Kiuchumi na Taratibu za Utoaji Leseni
Divisheni ya Uendelezaji na Uzalishaji
Divisheni ya Usimamizi wa Taarifa za Utafutaji na Uzalishaji
Divisheni ya Usalama wa Taarifa
Divisheni ya Afya na Usalama
Divisheni ya Mazingira
Divisheni ya Uratibu wa Shughuli za Bodi ya Mamlaka na Masuala ya Kesi
Divisheni ya Usimamizi wa Mikataba na Matekelezo
Divisheni ya Mipango na Tafiti
Divisheni ya Utawala na Rasilimali Watu
Divisheni ya Fedha
ZPRA ina vitengo 4 vinavyojitegemea ambavyo ni:



