ZAFIRI
Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini Zanzibar (Zanzibar Fisheries Research and Marine Resource Institute) – ZAFIRI, ni Taasisi mpya iliyoanzishwa tarehe 23 April, 2019 kwa Hati ya Sheria (Legal Notice) Nambari 32, chini ya kifungu 53 cha Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 na kifungu 55 cha Sheria ya Utumishi wa Umma, Act Nam. 2 ya mwaka 2011 kwa madhumuni ya kuendeleza tafiti za Uvuvi na Maliasili za baharini Zanzibar ili kuimarisha sekta ya Uvuvi, ukulima wa mazao ya baharini na uhifadhi wa mazingira ya Bahari nchini.
Dr. Zakaria Ali Khamis
Mkurugenzi mkuu ZAFIRI
Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini atakua ni mtendaji na msimamizi mkuu wa shughuli za kila siku za Taasisi. Mkurugenzi Mkuu anaeteuliwa na Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa mujibu wa kifungu Na. 24 (1) cha Hati ya Sheria nambari 32 ya kuanzishwa kwa Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini Zanzibar.
Kuwa kituo bora cha utafiti wa uvuvi, maliasili za baharini na sayansi za bahari katika eneo la ukanda wa Magharibi wa Bahari ya Hindi.
Kufanya tafiti za kisasa za uvuvi, rasilimali za bahari na sayansi za bahari, pamoja na kuendeleza mbinu na ubunifu bora ili kutoa muongozo wa matumizi endelevu ya rasilimali za bahari, maendeleo ya sekta za uvuvi na ukulima wa mazao ya baharini, na uhifadhi wa mazingira ya bahari.
Kwa mujibu wa Hati ya Sheria inayounda Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini ya mwaka 2019, kifungu namba 6(1) kimeipa mamlaka taasisi hii kuwa na majukumu yafuatayo:
Taasisi itakuwa na Idara nne (4) zifuatazo:
Taasisi itakuwa na Divisheni kumi (10) ambazo zitaongozwa na Wakuu wa Divisheni kwa mujibu wa muundo wa utumishi na wataripoti moja kwa moja kwa Wakurugenzi wa Idara kwa mujibu wa muundo wa Idara husika.
Divisheni hizo ni kama zifuatazo:
Aidha, Taasisi ya Utafiti wa Uvuvi na Maliasili za Baharini Zanzibar itakuwa na vitengo sita (6) vitakavyoongozwa na Wakuu wa Vitengo kwa mujibu wa muundo wa utumishi na vitakuwa vinaripoti moja kwa moja kwa Mkurugenzi Mkuu,vitengo hivyo ni kama vifuatavyo:



