Uendeshaji na Utumishi

IDARA YA

UENDESHAJI NA UTUMISHI

Idara ya Uendeshaji na Utumishi inahusika na utoaji wa huduma pamoja na kusimamia maslahi ya rasilimali watu ya Wizara, ikiwa ni pamoja na kutunza, kuhuisha na kuhifadhi kumbukumbu za Ofisi. Idara hii inaongozwa na Mkurugenzi ambae ni mteuliwa wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Nd. Issa Suleiman Ali
Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji na Utumishi

MAJUKUMU YA IDARA YA UENDESHAJI NA UTUMISHI

Kutoa huduma za uongozi wa Rasilimali watu na Utawala
Kusimamia masuala ya ajira, mafunzo, sifa za utendaji na kupandishwa vyeo
Kuweka kumbukumbu za wafanyakazi na kufanya tathmini ya kila muda ya utendaji
Kuhifadhi na kutunza kumbukumbu na rasilmali zote za Ofisi
Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa mkataba wa huduma kwa mteja
Kushughulikia na kukadiria upatikanaji wa mahitaji, vifaa na vitendea kazi
Kuandaa na kusimamia utekelezaji wa mkataba wa utoaji wa huduma kwa umma
Kusimamia nidhamu na maadili ya watumishi
Kutafsiri na kusimamia sheria, kanuni na miongozo ya kazi
Kuratibu utekelezaji wa upimaji wa utendaji kazi
SEHEMU ZA IDARA YA UENDESHAJI NA UTUMISHI

Idara ya Uendeshaji na Utumishi inaundwa na Divisheni tatu (3) ambazo ni:-

Divisheni ya Uendeshaji

Divisheni hii inahusika na masuala ya utawala, uendeshaji na usimamizi wa shughuli za kila siku za Ofisi

Divisheni ya Utumishi

Divisheni hii inahusika na masuala ya maendeleo na usimamizi wa rasilimali watu ndani ya Ofisi ikiwemo ajira, mishahara, mafunzo kwa watumishi, upimaji utendaji kazi pamoja na upandishaji vyeo

Divisheni ya Utunzaji wa Kumbukumbu

Divisheni hii itahusika na shughuli za uwekaji wa kumbukumbu na uhifadhi wa nyaraka na kazi mbali mbali za Ofisi

Categories

At vero eos et accusamus et iusto odio digni goikussimos ducimus qui to bonfo blanditiis praese. Ntium voluum deleniti atque.

Melbourne, Australia
(Sat - Thursday)
(10am - 05 pm)
Shopping Cart (0 items)
Translate »