Uvuvi na Maendeleo ya Mazao ya Bahari

  • Mwanzo
  • Uvuvi na Maendeleo ya Mazao ya Bahari
IDARA YA

UVUVI NA MAENDELEO YA MAZAO YA BAHARINI

Idara hii inahusika na kudhibiti na kuendeleza shughuli za uvuvi endelevu, kilimo cha mwani, na ufugaji wa viumbe maji kama vile Matango Bahari, Kaa Tope, na Samaki. Idara hii inaongozwa na Mkurugenzi ambae ni mteuliwa wa Mheshimiwa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi.

Nd. Issa Suleiman Ali
Mkurugenzi Idara ya Uendeshaji na Utumishi

MAJUKUMU YA IDARA YA UVUVI NA MAENDELEO YA MAZAO YA BAHARINI

Kusimamia tathmini mabli mbali za maendeleo ya shughuli za uvuvi na mazao ya baharini
Kusimamia ukusanyaji wa tozo na takwimu za uvuvi na mazao ya baharini
Kuinua uelewa wa jamii juu ya umuhimu wa uvuvi endelevu, miundombinu, zana bora, mitaji na masoko
Kusimamia utekelezaji wa sheria na kanuni za uvuvi endelevu
Kusimamia, kukuza, kuendeleza, kudhibiti na kufuatilia shughuli za uvuvi endelevu, kilimo cha mwani, na ufugaji wa viumbe maji
Kusimamia na kutekeleza mipango ya utekelezaji wa program za uvuvi na mazao ya baharini ikiwemo takwimu, elimu, nyenzo, miundo mbinu, viwanda, mitaji na masoko
SEHEMU ZA IDARA YA UVUVI NA MAENDELEO YA MAZAO YA BAHARINI

Idara ya Maendeleo ya Uvuvi inaundwa na Divisheni tatu (3) ambazo ni:

Divisheni ya Uvuvi

Divisheni hii inahusika na kuwawezesha na kuwajengea uwezo wavuvi wadogo kwa ajili ya kuimarisha Shughuli za Uvuvi nchini

Divisheni ya Ufugaji wa Viumbe vya Baharini

Divisheni hii inahusika na kusimamia na kuratibu shughuli za ufugaji wa Viumbe vya Baharini pamoja na kuanzisha mashamba ya mfano kwa kushirikiana na jamii katika ukuzaji wa sekta ya Uvuvi

Divisheni ya Ufugaji wa Viumbe vya Baharini

Divisheni hii inahusika na kuratibu shughuli za usarifu na ukuzaji masoko kwa mazao ya Baharini

Categories

At vero eos et accusamus et iusto odio digni goikussimos ducimus qui to bonfo blanditiis praese. Ntium voluum deleniti atque.

Melbourne, Australia
(Sat - Thursday)
(10am - 05 pm)
Shopping Cart (0 items)
Translate »